KARIBU SANA RAFIKI YETU MUNGU ANATAKA KUKUSAIDIA KAMA UKOTAYARI KUPOKEA MSAADA WAKE KUPITIA SEHEMU HII UNANAYOISOMA SASA HIVI ZAIDI YA MASOMO PIA UNARUHUSIWA KUPIGA SIMU KWA MSAADA WA USHAURI NA MAOMBEZI HUDUMA HII NI BURE KWA MTU YEYOTE, 0756 809 209 ITAPOKELEWA NA YULE MTU WA MUNGU NABII SAMSON MBOYA

Blogger news

Wednesday, February 4, 2015

On Wednesday, February 04, 2015 by Mtumishi wa mungu na mkewe, samson mboya

VIPENGELE9VYA MAOMBI

 

 

Na Mtu wa Mungu Nabii Samson Mboya,

 

 SOMO VIPENGELE 9 VYA MAOMBI

Utangulizi:

Maisha ya mwanadamu Muongozo mzima wa kuishi kwetu tunaupata kutoka katika kitabu kitakatifu yaani Bibilia Takatifu maombi ya watu wengi hayajibiwi kwakuwa hayana kanuni maombi yanakanuni na misngi,kanuni nivileunavyoelewa Neno kwa undani,msingi ni Neno lenyewe,Yesu akawafundisha wanafunzi wake kuomba Mathayo 6:9, sala hii niamtukuza Mungu imebeba msamaha,chakula cha kila siku na mahitaji yote, ila kuna Zaidi ya hayo hebu tuangalie maandiko  Zaidi,

 YOHANA 14:14-31 14:13-31.  Katika mistari hii, pamoja na mambo mengine, tutajifunza kuhusu, Namna ya kuomba“. 

 (1)                          KUOMBA KWA JINA LA YESU (MST. 13-14)

Yesu Kristo aliye Bwana na Mwalimu wetu, hapa anatufundisha jinsi ya kuomba, ili maombi yetu yawe na uwezo wa kipkee wa kuleta majibu kutoka kwa Mungu.  Anatuelekeza kumwomba Mungu baba, kwa JINA LA YESU, na anarudia maelekezo haya tena na tena (YOHANA 16:23-24).  Shetani, adui yetu, hataki tuombe kama tulivyo elekezwa kuomba , hivyo mbinu yake kubwa, ni kutufanya tuombe kinyume na maelekezo ya Yesu. 

1.1                          Muovu anafahamu Nguvu iliyo katika Jina la Yesu

Hataki tuombe kwa usahihi anataka tuwaombe watakatifu Petro, Yohana, Yakoba, n.k.  Watuombee.  Yote haya, ni kinyume na maelekezo haya ya Yesu.  Maelekezo ya Yesu kwetu ni “Nanyi Mkiomba“,.  Wanaotajwa kutuombea katika Biblia, ni wawili tu hapa Roho Mtakatifu na Yesu mwenyewe; (MATENDO 1:13-15).  Kutumia sanamu za watakatifu fulani katika maombi yetu,  hivyo ni kinyume na maelekezo haya.  Mungu ni Roho, inatupasa kumwabudu KATIKA ROHO NA KWELI, na kuikimbia ibada ya sanamu, maana sanamu au Kuabudu mizimu,hizi ni dhambi mbele za Mungu Hii ni pamoja na kushiriki kupiga ramli, n.k (ISAYA 31:7; ZABURI 135:15-18; 1 WAKORINTHO 10:14).

(2)                          HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI (MST. 13-14)

 

Yesu Kristo hapa anatuelezea juu ya hakika ya kujibiwa maombi.  Anasema, tukiomba kama alivyotuelekeza kwa Jina la Yesu, hilo tunaloliomba, atalifanya.  Hata hivyo, hatuna budi kuviondoa vikwazo vingine vya kujibiwa maombi, vinavyotajwa katika maandiko, ili hakika ya kujibiwa maombi itende kazi kwetu.  Hatuna budi kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu au Neno lake (1 YOHANA 5:14-15; MATHAYO 20:20-23).  Hatuna budi pasipo kutaka kuvitumia kwa tamaa zetu (YAKOBO 4:3).  Hatuna budi kuomba pia kuwa mbali na dhambi au uasi wa sheria za Mungu (MITHALI 28:9; 15:29; YAKOBO 4:2-7), na pia hatuna budi kuomba kwa imani, pasipo shaka yoyote (YAKOBO 1:6-7).  Tukiondoa vikwazo hivi, hatuna budi kuwa na hakika ya kujibiwa maombi kwa wakati wa Mungu uliokubalika.

(3)                            ALAMA YA KUMPENDA YESU (MST. 15, 21, 23-24)

Wako watu wengi ambao wanassema wanampenda Yesu, hata hivyo, wengi kati yao wanapenda kwa neno tu, siyo kwa tendo na kweli (1 YOHANA 3:18).  Yesu anatufundisha alama itakayoonyesha kwa tendo na kweli kwamba tunampenda Yesu.  Alama hii, ni kuzishika amri zake zote, kulishika neno lake na kulitendea kazi kama lilivyo, bila kulijadili.  Yeyote anayesema anampenda Yesu huku hayashiki maneno yake, huyu ni mwongo. Na lazima ufahamu kama wewe ni mwongo ujuwe unamtumikia shetani maana maandiko yanatufundisha wazi, kila atendaye dhambi ni wa ibilisi na ibilisi ni Baba wa uwongo, ili kuomba unahitaji kusaidiwa,

(4)                          Msaidizi wa maombi yetu (MST. 16-17, 25-26)

Yesu Kristo alipokuwa duniani, alikuwa Msaidizi wa kipekee kwa wanafunzi wake.  Hata sasa anatusaidia sisi (2 WAKORINTHO 6:2; WAEBRANIA 2:18; 13:6).  Kabla ya kuondoka, anatutambulisha kwa Msaidizi mwingine.  Msaidi huyu, siyo Mtume Mohamed, kama wengine wanavyodai.  Msiaidizi huyu, ni ROHO WA KWELI, siyo mtu.  Ulimwengu hauwezi kumpokea, wala kumwona kwa macho, wala kumtambua; naye atakuwa NDANI ya wanafunzi wa Yesu, naye anakaa nao MILELE (MST. 16-17).  Sifa hizi zote, haziko kwa mtume yeyote mwanadamu.  Wengine wote hawakuwa ndani ya watu na pia hawakukaa milele!  Msaidizi huyu wingine ni ROHO MTAKATIFU (MST. 25-26).  Huyu hutusaidia udhaifu wetu wa kuomba (WARUMI 8:26), na kutufundisha na kutukumbusha yote, na kutuongoza atutie kwenye kweli yote.  Msaidizi huyu, ni wa muhimu mno kwetu ikiwa tunataka kuwa mashahidi wa Yesu (MATENDO 1:8).  Pasipo Msaidizi huyu, hatuwezi kuwaleta watu kwa Yesu kwa mfanikio makubwa (YOHANA 16:7-8).

(5)                          SITAWAACHA NINYI YATIMA (MST. 18-20)

Yesu hakutuacha yatima.  Siyo tu ametuachia Msaidizi mwingine, lakini tukiwa wawili watatu tumekusanyika kwa jina lake, yupo kati yetu katika roho (MATHAYO 18:20).  Kwa sasa tunamwona katika roho, hata hivyo atakuja kwetu wakati wa kunyakuliwa kwa kansia na tutamwona katika utukufu wake akiwa ndani ya Baba.

(6)                          FAIDA ZA KUZISHIKA AMRI ZA YESU (MST. 21-23)

Tukizishika amri za yesu, Baba na Mwana wote hutupenda.  Yesu akitupenda hivi, anajidhihirisha kwetu; kutuonyesha upendo wake katika kututendea mengi, katika roho na mwili.  Tukizishika amri za Yesu, Baba na Mwana, hufanya makao kwetu.  Wakifanya makao kwetu, hatutapungukiwa kitu, wala hatuna haja tena ya kuogopa lolote.

(7)                          MSIWE NA WOGA (MST. 27-29)

Woga, ni kinyume na imani (MARKO 4:40).  Woga hautokani na Mungu, bali Shetani (2 TIMOTHEO 1:7).  Tukiruhusu woga au hofu kututawala, tunampa Ibilisi nafasi ya kutupa adhabu (WAEFESO 4:27; 1 YOHANA 4:18).  Ikiwa baba, Mwana, wamefanya makao kwetu, na roho Mtakatifu pia yuko ndani yetu, na ni Msaidizi wetu, kwa nini tuogope kama kwamba tuko wenyewe?  Yesu kwa kutupa maelezo haya, anazidi kusema “Amani yangu nawapa“, Amani nawaachieni“.  Amani yake Yesu aliyotupa, itafuta kila namna ya hofu ndani yetu.  Kama tuna hofu, tupokee amani hii ndani mwetu, kwa imani.

(8)                          MKUU WA ULIMWENGU HUU HANA KITU KWA YESU (MST. 30)

Mkuu wa Ulimwengu huu yaani watu wa ulimwengu huu wenye dhambi, ni Ibilisi au Shetani (1 YOHANA 5:19; WAEFESO 2:1-2; WAKOLOSAI 1:13).  Yesu hapa, anatuhakikishia kwamba Shetani hana kitu chochote kwake.  Tunapoomba na kuliitia Jina la Yesu, hatuna haja ya kuogopa, Shetani hana kitu kwa Bwana wetu Yesu!  Majini yote hayana kitu kwake.  Hatuna haja ya kuogopa vitisho vya mapepo tukiwa na Yesu!

 (9)                          JINSI YA KUUJULISHA ULIMWENGU YA KUWA TUNAMPENDA BABA (MST.

Hapa, Yesu anatuonyesha jinsi ya kuujulisha ulimwengu ya kuwa tunampenda Baba.  “Kama Baba  alivyomwamuru, ndivyo afanyavyo“, ni kielelezo cha Yesu kwetu.  Je, kama baba anavyotuamuru katika neno lake, ndivyo tufanyavyo?  Kama sivyo, hatumpendi..

************************************************************************

Je Unataka kuingia mbinguni?  Ni utakatifu tu siyo cheo cha kanisa flani wala siyo ujuzi elimu ya mtu(WAEBRANIA 12:14).  Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27).  Kinyonge ni kipi?  Ni yule anayetenda dhambi.  Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge!  Je, wewe ni mtakatifu?  Jibu ni la!

 Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema wewe ni Mkristo na kanisani unakwenda sadaka na mafungu ya kumi unatoa bado;  wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13;  YOHANA 14:6).  Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii?  Tafuta Mchungaji  akusaidie kukupa muongozo wa  sala ya toba

Ikiwa unahitaji msaada Zaidi wa ushauri na maombezi

Usisite kuwasiliana na Mtu wa Mungu Nabii  Samson Mboya

Piga simu 0756 809 209 huduma hii ni bure,