Thursday, September 29, 2016
On Thursday, September 29, 2016 by Mtumishi wa mungu na mkewe, samson mboya
Ujimbe watu waliyowekewa mipaka ya kutofanikiwa
Utangulizi
Kuna watu wengi Sana hatima zao zimewekewa mipaka
na hiyo ndiyosababu kubwa maisha yao kuwa vile yalivyo leo unaweza kujiwekea
mipaka wewe mwenyewe kwa tabia yako bila kujuwa, wazazi kwakukulaani,watu
waliokuzungukaau kwakulogwa,kukosa ufahamu wa kiMungu
zao maarifa imeandikwa Daniel 2; 20 hata katika kuteseka imeandikwa Hosea 4;6
Tofauti nyingine ya mtu na Mtu ni Matumizi ya
akili zake juu ya kile anachokitaka, kufanya, kusema, kuona, kusikia,
Kuna watu akili zao zimewekewa mipaka na mapepo
kiasi kwamba wanafikiria wamefika
mwisho,wakuishi,kufanikiwa,kusoma,biashara,kazi, kuoa au kuolewa kumbe bado
mwisho ule mpaka ndiyo unaomtesa
kuendelea na safari,
Mstari
wa kukumbuka Daniel 2; 20
Mpaka ni kizuwizi kinacho zuwia kati ya pande
mbili ili jambo la upande mmoja lisiende upande mwingine
AINA ZA MIPAKA ANAYOWEZA KUWEKEWA MTU
Mpaka ni makubaliano baina ya pande mbili juu ya
uhuru wa jambo flani, mpaka wa kwanza ni wa kiroho,na wakimwili
Mpaka unaweza kuwa wa maneno,au maandishi,au kitu
ila kiuhalisia mpaka unaanzia rohoni na
unaishia rohoni kwa alama za mwilini,
- Kuna watu akili imewekewa mipaka ya kufikiria
- Kuna watu wamewekewa mipaka kwa kulaaniwa
- Kunawatu akili waliyowekewa mipaka kwa vitisho
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka kwa zawadi flani
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka kwa ahadi nyingi nzuri anabaki kusubiri uzee unamkuta bado anasubiri
- Kuna watu akili wamewekewa mipaka kwa kutishiwa na jamii, eneo, mazingira.
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka ya magonywa ya mapepo
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka ya kibri cha mapepo
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka ya ujinga wa kimapepo
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka ya roho za mizimu
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka kwa kulogwa
- Kunawatu akili wamewekewa mipaka ili wao wafanikiwe kichawi
- Kuna watu akili wamewekewa mipaka ya stress,
Sasa kuna kifungo ambacho unaweza kumwona mtu yuko
vizuri lakini akili yake imefungwa. Sasa kwanini mungu ametupa akili ni
kwasababu kuna mambo mengine tunaweza kuyafanya kwa akili tu Unaweza
kumshuhudia mtu anakwambia jambo flani hadi ukamshangazwa kumbe akili imewekewa
mpaka na mapepo ndio maana mungu
alivyowaumba watu akaweka mambo mengine tusimsumbue ila tutumie akili zetu.
MFANO:
Maisha tunayoishi Mungu aliyawekea utaratibu namna ya kuishi kujilinda na
uovu,kuishi kwa kumtii Mungu, kuisikia sauti ya Mungu Kumb 28:1 Unahitaji
Baraka za wapi shambani,mjini,kazini,familia
AKILI
YA DARASANI NA YA MTAANI INAHITAJI UTOFAUTI KIDOGO
Akili ya masomo na akili ya mtaani
Mtu anaweza kusoma vizuri sana akija kwenye upande
wa kutunza familia akaanza darasa jipya na baadhi ya mitihani asipokuwa makini
akapata sifuri, watu wanabaki kusema mbona amesoma sana?uvumilivu wa masomo na
uvumilivu wa ndoa nitofauti kidogo Akili
inaweza kuwekewa mipaka na mapepo, kama umewahi kusikia watu wakisema
amekamatwa masikio
Imeandikwa
“enyi waume ishini na wake zenu kwa akili” unakuta mtu
anaakili ya bihashara kutunza familia yake anashindwa, anaakili ya kufanya kazi
kwa ufanisi mkubwa,hata eneo lake la kazi anaongoza mamia ya watu kazini ila
mke au mme mmoja anamshinda kunasehemu kunampaka
anahitaji msaada, wa ushauri na maombi
Hii ndiyo sababu ninashawishika kukushauri wewe
kumpokea Yesu awe bwana na muokozi wa maisha yako ili kupata ufahamu Mpya ili
kila kitu kiwe kipya kilichozaliwa na
roho ni roho,
Imeandikwa
Mithali 3:19 kwa hekima bwana aliiweka misingi ya
nchi; kwa akili zake akazifanya mbingu imara;
Kuna watu wakianza
kufikiria mambo ya maana wanaumwa akili na wengine wanahela mkonononi lakini
hawajui jinsi ya kizitumia na kuna watu wanatumia akili za watu kufikiria na kufanya
maamuzi na wengine wameibiwa akili zao hawawezi kufanya mambo ya maendeleo yake
anatajirisha wengine, kila kukicha mwisho akili yake inarudi arithini
Hii ndiyo sababu makaburini kunakuwa na
dhamani kubwa sababu watu wanalala na akili ikiwa haijatumika kabisa na hakuna
mtu wakuja kuzitumia wengine wanajipa moyo mtoto wangu atakuwa jembe, kama wewe
ulikuwa ndiye mzazi ukawa mpini mtoto atatoa wapi uwezo wa kuwa jembe na
umemjengea msingi gani wa yeye kuwa vile unavyofikiria wewe nayeye kuna Hatari
ya kuzikwa na akili zake zote, Imeandikwa Hosea
4:6.
Unapokataliwa na Mungu unageuka mali ya ibilishi
utaanza kuishi maisha mapya ya utumwa na mateso waibilisi (wachawi) wanaweza
kuloga akili ya Mtu, akashindwa kufikia malengo,
Imeandikwa
Wagalatia 3:1-enyi wagalatia msio na akili, ni nani
aliyewaloga, ninyi ambao yesu kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa
amesulibiwa?
Imeandikwa
Kutoka 7:11 ndipo farao naye akawaita wenye akili
na wachawi; na hao waganga wa misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.
Wenye akili wanauwezo kuliko wachawi na waganga,
akili ya kumwambia mtu jambo akalifahamu na kukubaliana nalo hiyo ni akili ya
mtu.
Akili
iliyohuru ni ya dhamani sana,
Maisha mazuri unayoyataka hutakiwi kumuuliza Mungu
Unachotakiwa ni kutumia akili kama haijawekewa mipaka Mungu ni wautaratibu
usipopata ufahamu unaweza kukaa unassubiri Mungu waka Mungu nay eye anakusubiri
wewe,
Biblia
inasema mtu akizaliwa akaishi miaka mia asipate chakula kizuri na asiishi
vizuri ni afadhali mimba iliyoharibika.
Kutoka
35:35 amewajaza watu hao akili za moyoni, ili watumike
katika kazi kila aina, ya mwenye kuchora mawe, na kazi ya werevu, na ya mwenye
kutia taraza, katika nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na
nyekundu, na kitani nzuri, na ya mwenye kufuma nguo; ya hao wafanyao kazi yo
yote, na ya wenye kuvumbua kazi za werevu.
Mungu alikuwa anamwambia musa katikati yako
nimewaweka watu wenye akili wanaoweza kufanya mambo makubwa.
Kumbukumbu
ya torati 1:15
15 basi nikatwaa vichwa vya kabila zenu wenye akili,
waliojulikana, nikawafanya wawe vichwa juu yenu, maakida ya elfu elfu, na
maakida ya mia mia, na maakida ya hamsini hamsini, na maakida ya kumi kumi, na
wenye amri, kwa kadiri ya kabila zenu.
Kama akili imefungwa unaweza ukaenda kaburini na
akili ikiwa bikra.
DALILI ZA AKILI ILIYOWEKEWE MIPAKA
1
mambo ya nyakati12:32
35. na wa wana wa isakari, watu wenye akili za
kujua nyakati, kuyajua yawapasayo israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu
mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
Akili ya mtu inaweza kuwekewa mpaka ili isifikirie
maendeleo anayoyataka
1.
Akili yako inapanga mipango ambayo wewe hutaki na hujawahi kuwaza
kuifanya, mipango inayopangwa kule kwenye akili yako inakujia na wewe umekaa na
hujawahi kufanya hiyo unayoiwaza si rahisi
2.akili iliyo wekewa mipaka apoanza kupanga mipango ya maendeleo kichwa
kinauma,au kuchanganyikiwa na anashindwa
kuendelea kufikiria au hasira inamtawala kabisa bila sababu,
3. Akiawaza jambo litakalompa mafanikio mazuri
gafla anahisi uwoga,wa kushindwa,
4. Anaanzisha miradi mingi kwa garama kubwa utekelezaji
ni hakuna
5. Unaota kila mara ndoto za mafanikio ila
zinabaki katika mawazo mazuri na simulizi
6. Unakuwa na shahuku ya kufanya jambo flani au
kuwa kama flani ila hofu inakufunika mwisho unakuwa msimulizi
7. Kila unalolianzisha au kujaribu unajilinganisha
na mtu flani ndugu au jamaa wa karibu aliyeshindwa
8. Ukifanya jambo likikaribia kufanikiwa basi
linakuja wazo la matumizi makubwa au uharibifu flani amba hata wewe
hujatarajia,
Shule inaongeza maarifa akilini ila kutumia
maarifa uliyonayo kufanya kile unachokitaka ni habari nyingine mtu kukaa pale alipo
na kuridhika ni moja ya mpaka,
Mfano mwanzilishi wa kampuni ya simu za apple mr
stivi kama angekufa kabla hajatoa simu ya apple ungeenda kule kaburi ya inchi
yake ungeona simu zote za apple zimelala kaburini kama una macho ya rohoni. Sio
kiwango cha elimu kinakutambulisha wewe bali ni kiwango cha akili ile utakayoitumia
ndiyo itakutambulisha na watu kusema anaakili sana mtu huyu
Inawezekana
akili yako inatumiwa sehemu flani na wewe hunufaiki hata kidogo ushauri wangu
unahitaji maombi ya kurudisha wizi huo wa akili yako,
Yeyote anayeimarisha utawala ufalme wake Kwa
kutumia akili yangu ninawateka nyara kwanzia sasa maana imeandikwa Yeremia
30:16
Hata Kama wameibiwa akawekewa mipaka panahitajika
maombi maalumu ya kupanua mipaka yao wawe huru Isaya 42:22 watu walioibiwa na
kutekwa’ ninaamuru akili iliyoibiwa irudi Kwa jina la yesu kristo kwa damu ya
yesu. Katika jina la yesu nabomoa ngome inayozuia akili kwa damu ya yesu.
Naondoa wigo uliowekwa kwenye akili yangu kwa jina la yesu, naondoa wigo wa
hofu, naondoa wingi wa mashaka kwa damu ya yesu.
Lazima kubomoa ukuta waliowekewa kwamba
wasiolewe,wasifanye biashara inchi za njie,wasiolewe au kuoa,wasisome
sana,wasipate nafasi ya uongozi,wasikubalike katika jamii, wasiishi maisha yao
halisi,wasiwe walikotakiwa kuwa,
Katika jina la Yesu,
Search
Popular Posts
-
Na Mtu wa Mungu Nabii Samson Somo : KUHARIBU MADHABAHU YA ADUI JUU YA MAISHA YAKO Utangulizi Kimsingi kufanikiwa au kuharib...
-
Maombi ya kupinga Roho ya mauti, 2Wafalme 4:40 Utangulizi: Roho ya mauti unaweza kuipinga kwa maombi isaya 38:1 ...
-
VIPENGELE 9 V YA MAOMBI Na Mtu wa Mungu Nabii Samson Mboya, SOMO VIPENGELE 9 VYA MAOMBI Utangulizi: Maisha...
-
Kuuoshwa miguu Yohana 13:3-8 Utangulizi Yesu, hali akijua ya kuwa Baba amempa vyote mikononi mwake, na ya kuwa alitok...
-
Ujimbe watu waliyowekewa mipaka ya kutofanikiwa Utangulizi Kuna watu wengi Sana hatima zao zimewekewa mipaka na hiyo ndiyosababu k...
-
MAUTI YA KUTOSAMEHE Warumi 6: 23 Utangulizi: Watu wengi wamekufa kiroho au kimwili kwasababu ya kutokusamehe na kuachilia wengine ...
Recent Posts
Blog Archive
Powered by Blogger.